يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنَّ وَعۡدَ ٱللَّهِ حَقّٞۖ فَلَا تَغُرَّنَّكُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَا وَلَا يَغُرَّنَّكُم بِٱللَّهِ ٱلۡغَرُورُ
Enyi watu! Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni ya kweli. Basi yasikudanganyeni maisha ya dunia, wala mdanganyifu asikudanganyeni juu ya Mwenyezi Mungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi watu! Hakika agizo la Mwenyezi Mungu la Ufufuzi, malipo mema na mateso ni kweli iliyothibiti, basi yasiwadanganye maisha ya duniani kwa matamanio yake na matakwa yake, wala asiwadanganye Shetani kuhusu Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس