مِّن وَرَآئِهِمۡ جَهَنَّمُۖ وَلَا يُغۡنِي عَنۡهُم مَّا كَسَبُواْ شَيۡـٔٗا وَلَا مَا ٱتَّخَذُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ أَوۡلِيَآءَۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٌ
Na nyuma yao ipo Jahannamu. Na walio yachuma hayatawafaa hata kidogo, wala walinzi walio washika badala ya Mwenyezi Mungu. Na watapata adhabu kubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Basi mbele ya hao wenye kuzifanyia shere aya za Mwenyezi Mungu patakuwa na moto wa Jahanamu. Na hakitawafalia wao kitu chochote kile walichokichuma cha mali na wana wala waungu wao waliowaabudu badala ya Mwenyezi Mungu. Na watakuwa na adhabu kubwa yenye uchungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس