ثُمَّ جَعَلۡنَٰكَ عَلَىٰ شَرِيعَةٖ مِّنَ ٱلۡأَمۡرِ فَٱتَّبِعۡهَا وَلَا تَتَّبِعۡ أَهۡوَآءَ ٱلَّذِينَ لَا يَعۡلَمُونَ
Kisha tukakuweka wewe juu ya Njia ya haya mambo, basi ifuate, wala usifuate matamanio ya wasio jua kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kisha tukakufanya, ewe Mtume, uwe kwenye njia iliyofunuka wazi kuhusu jambo la Dini. Basi fuata Sheria ambayo Mwenyezi Mungu Amekupatia, na usifuate matamanio ya wajinga wa Sheria ya Mwenyezi Mungu, wasiojua haki. Katika hii aya kuna ushahidi mkubwa juu ya ukamilifu wa Dini hii na utukufu wake na ulazima wa kufuata hukumu zake na kutopotoka kuelemea kwenye matamanio ya makafiri na wapotofu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس