إِنَّهُمۡ لَن يُغۡنُواْ عَنكَ مِنَ ٱللَّهِ شَيۡـٔٗاۚ وَإِنَّ ٱلظَّـٰلِمِينَ بَعۡضُهُمۡ أَوۡلِيَآءُ بَعۡضٖۖ وَٱللَّهُ وَلِيُّ ٱلۡمُتَّقِينَ
Kwa hakika hao hawatakufaa kitu mbele ya Mwenyezi Mungu. Na hakika wenye kudhulumu ni marafiki wao kwa wao. Na Mwenyezi Mungu ni rafiki wa wamchao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hawa waliomshirikisha Mola wao wanaokuita ufuate matamanio yao, hawatakufalia kitu, ewe Mtume, kwa kukuepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu iwapo umefuata matamanio yao. Na hakika madhalimu wenye kukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu miongoni mwa wanafiki, Mayahudi na wasiokuwa hao wanasaidiana wao kwa wao dhidi ya wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na walio watiifu Kwake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwapa ushindi wenye kumcha Mola wao kwa kutekeleza faradhi Zake na kujiepusha na makatazo Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس