أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ حَقَّ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقَوۡلُ فِيٓ أُمَمٖ قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِهِم مِّنَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ خَٰسِرِينَ
Hao ndio ambao imehakikikishwa hukumu juu yao kama mataifa yaliyo kwisha pita kabla yao miongoni mwa majini na watu. Hakika hao wamekuwa wenye kukhasiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hao ambao sifa zao ni hizi imepasa juu yao adhabu ya Mwenyezi Mungu, na yamewashukia mateso Yake na hasira Zake, wakiwa ni katika jumla ya ummah waliopita kabla yao, miongoni mwa majini na binadamu, waliokuwa kwenye ukafiri na ukanushaji. Kwa kweli wao ni wenye hasara kwa kuchagua upotevu na kuacha uongofu, na kuchagua adhabu na kuacha starehe.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس