وَمَن لَّمۡ يُؤۡمِنۢ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ فَإِنَّآ أَعۡتَدۡنَا لِلۡكَٰفِرِينَ سَعِيرٗا
Na asiye muamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi kwa hakika Sisi tumewaandalia makafiri Moto mkali.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na asiyemuamini Mwenyezi Mungu na yale aliyokuja nayo Mtume Wake, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na akazifuata Sheria Zake kivitendo, basi huyo ni kafiri anayestahili kuteswa, kwani hakika sisi tumewaandalia makafiri adhabu yenye kuunguza ndani ya Moto.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس