فَضۡلٗا مِّنَ ٱللَّهِ وَنِعۡمَةٗۚ وَٱللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٞ
Kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na neema zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye hikima.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kheri hii walioipata ni nyongeza njema kutoka kwa Mwenyezi Mungu juu yao na ni neema. Na Mwenyezi Mungu Anamjua sana anayezishukuru neema Zake, ni Mwingi wa hekima katika kuendesha mambo ya viumbe Vyake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس