مَّن ذَا ٱلَّذِي يُقۡرِضُ ٱللَّهَ قَرۡضًا حَسَنٗا فَيُضَٰعِفَهُۥ لَهُۥ وَلَهُۥٓ أَجۡرٞ كَرِيمٞ
Ni nani atakaye mkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mwema, ili amrudishie mardufu, na apate malipo ya ukarimu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ni yupi yule anayetoa katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa kutaka thawabu kutoka ndani ya moyo wake bila kusimanga wala kuudhi, ili Amuengezee Mola wake malipo na thawabu na apate malipo mema nayo ni Pepo?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس