وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِٱللَّهِ وَرُسُلِهِۦٓ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلصِّدِّيقُونَۖ وَٱلشُّهَدَآءُ عِندَ رَبِّهِمۡ لَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ وَنُورُهُمۡۖ وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَآ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَحِيمِ
Na walio muamini Mwenyezi Mungu na Mitume wake, hao ndio Masidiqi na Mashahidi mbele ya Mola wao Mlezi. Wao watapata malipo yao na nuru yao. Na walio kufuru na wakakadhibisha Ishara zetu, hao ndio watu wa Motoni.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mitume Wake na wasimbague yoyote miongoni mwao, hao ndio wakweli iliyokamilika imani yao kwa kile walichokuja nacho Mitume, kiitikadi, kimaneno na kivitendo, na ndio mashahidi mbele ya Mola wao; watapata malipo yao mengi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na nuru yao kubwa Siku ya Kiyama. Na wale waliokufuru na kukanusha dalili zetu na hoja zetu, wao ndio watu wa Motoni, hawatakuwa na malipo mema wala nuru.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس