ءَامِنُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَأَنفِقُواْ مِمَّا جَعَلَكُم مُّسۡتَخۡلَفِينَ فِيهِۖ فَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنكُمۡ وَأَنفَقُواْ لَهُمۡ أَجۡرٞ كَبِيرٞ
Muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake; na toeni katika alivyo kufanyeni nyinyi kuwa ni waangalizi wake. Basi walio amini miongoni mwenu, na wakatoa, wana malipo makubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na mtoe katika mali amabayo Mwenyezi Mungu Amewaruzuku na Akawafanya nyinyi ni wasimamizi wa mali hayo. Basi wale walioamini miongoni mwenu, enyi watu, na wakatoa mali yao watapata malipo makubwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس