إِنَّمَآ أَمۡوَٰلُكُمۡ وَأَوۡلَٰدُكُمۡ فِتۡنَةٞۚ وَٱللَّهُ عِندَهُۥٓ أَجۡرٌ عَظِيمٞ
Hakika mali yenu na watoto wenu ni jaribio. Na kwa Mwenyezi Mungu upo ujira mkubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hayakuwa mali yenu na watoto wenu isipokuwa ni majaribio na mtihani kwenu. Na Mwenyezi Mungu, Kwake Yeye kuna thawabu kubwa kwa aliyechagua kumtii Yeye kuliko kumtii asiyekuwa Yeye na akatekeleza haki ya Mwenyezi Mungu katika mali yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس