وَلَقَدِ ٱسۡتُهۡزِئَ بِرُسُلٖ مِّن قَبۡلِكَ فَأَمۡلَيۡتُ لِلَّذِينَ كَفَرُواْ ثُمَّ أَخَذۡتُهُمۡۖ فَكَيۡفَ كَانَ عِقَابِ
Na hakika walifanyiwa kejeli Mitume walio kuwa kabla yako. Na nikawapururia wale walio kufuru, kisha nikawashika! Basi ilikuwaje adhabu yangu!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na iwapo wameufanyia shere ulinganizi wako, ewe Mtume, basi kuna ummah kabla yako waliwafanyia shere Mitume wao. Basi usiwe na masikitiko, niliwapa muhula wale waliokufuru kisha nikawapatiliza kwa mateso yangu; na yalikuwa ni mateso makali.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس