۞مَّثَلُ ٱلۡجَنَّةِ ٱلَّتِي وُعِدَ ٱلۡمُتَّقُونَۖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۖ أُكُلُهَا دَآئِمٞ وَظِلُّهَاۚ تِلۡكَ عُقۡبَى ٱلَّذِينَ ٱتَّقَواْۚ وَّعُقۡبَى ٱلۡكَٰفِرِينَ ٱلنَّارُ
Mfano wa Bustani waliyo ahidiwa wachamngu, kati yake inapita mito, matunda yake ni ya daima, na pia kivuli chake. Huu ndio mwisho wa wale walio walio jilinda. Na mwisho wa makafiri ni Moto.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sifa ya Pepo ambayo Mwenyezi Mungu Amewaahidi nayo wale wanaomuogopa na kwamba mito inapita chini ya miti yake na majumba yake ya fahari, Matunda yake hayamaliziki na kivuli chake hakiondoki. Malipo mema hayo ya Pepo ndio mwisho wa waliomuogopa Mwenyezi Mungu wakajiepusha na mambo ya kumuasi na wakatekeleza faradhi Zake. Na mwisho wa makafiri ni Moto.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس