أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّا نَأۡتِي ٱلۡأَرۡضَ نَنقُصُهَا مِنۡ أَطۡرَافِهَاۚ وَٱللَّهُ يَحۡكُمُ لَا مُعَقِّبَ لِحُكۡمِهِۦۚ وَهُوَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ
Je! Hawakuona kwamba tunaifikia ardhi tukiipunguza nchani mwake? Na Mwenyezi Mungu huhukumu, na hapana wa kupinga hukumu yake, naye ni Mwepesi wa kuhisabu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kwani hawaoni hawa makafiri kwamba sisi tunaijia ardhi na kuipunguza pambizoni mwake kwa kuwapa Waislamu ushindi wa kuiteka miji ya makafiri na kuishikanisha na miji ya Kiislamu? Na Mwenyezi Mungu Anaamua, hakuna Mwenye kuurudi uamuzi Wake na hukumu Yake. Na Yeye ni Mpesi wa kuhesabu, basi wasifanye haraka ya kutaka kuletewa adhabu, kwani kila lenye kuja liko karibu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس