وَإِذۡ قَالَ لُقۡمَٰنُ لِٱبۡنِهِۦ وَهُوَ يَعِظُهُۥ يَٰبُنَيَّ لَا تُشۡرِكۡ بِٱللَّهِۖ إِنَّ ٱلشِّرۡكَ لَظُلۡمٌ عَظِيمٞ
Na Luqman alipo mwambia mwanawe kwa kumpa mawaidha: Ewe mwanangu! Usimshirikishe Mwenyezi Mungu. Kwani hakika ushirikina bila ya shaka ni dhulma iliyo kubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kumbuka na utaje, ewe Mtume, ushauri wa Luqman kwa mwanawe alipomuambia kwa kumwaidhia, «Ewe mwanangu! Usimshirikishe Mwenyezi Mungu ukajidhulumu nafsi yako, hakika ushirikina ni dhambi kubwa na ovu kabisa la madhambi makubwa.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس