يَٰبُنَيَّ إِنَّهَآ إِن تَكُ مِثۡقَالَ حَبَّةٖ مِّنۡ خَرۡدَلٖ فَتَكُن فِي صَخۡرَةٍ أَوۡ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ أَوۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ يَأۡتِ بِهَا ٱللَّهُۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَطِيفٌ خَبِيرٞ
Ewe mwanangu! Kikiwapo kitu cha uzito wa chembe ya khardali kikawa ndani ya jabali au ndani ya mbingu au ndani ya ardhi, basi Mwenyezi Mungu atakileta. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyo fichika, Mwenye khabari za yote.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Ewe mwanangu! Jua kwamba uovu au wema uwapo ni kadiri ya chembe ya hardali, nayo ni ile iliyo upeo wa udogo, iliyo ndani ya jabali au iliyo mahali popote, mbinguni au ardhini, Mwenyezi Mungu Ataileta Siku ya Kiyama na Ataihesabu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja Wake, ni Mtambuzi wa matendo yao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس