وَأَقۡسَمُواْ بِٱللَّهِ جَهۡدَ أَيۡمَٰنِهِمۡ لَئِن جَآءَهُمۡ نَذِيرٞ لَّيَكُونُنَّ أَهۡدَىٰ مِنۡ إِحۡدَى ٱلۡأُمَمِۖ فَلَمَّا جَآءَهُمۡ نَذِيرٞ مَّا زَادَهُمۡ إِلَّا نُفُورًا
Na waliapa kwa Mwenyezi Mungu ukomo wa kuapa kwao, kwamba akiwajia mwonyaji bila ya shaka watakuwa waongofu zaidi kuliko taifa jingine lolote. Lakini alipo wajia mwonyaji hakuwazidishia ila kuikimbia hiyo Haki,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wakanushaji wa Kikureshi waliapa kwa Mwenyezi Mungu viapo vikali kwamba wakijiwa na mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu wa kuwaonya mateso ya Mwenyezi Mungu, watakuwa ni wenye kusimama wima zaidi na wenye kufuata haki zaidi kuliko Mayahudi, Wanaswara na wengineo. Na alipowajia Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, hilo halikuwaongezea wao isipokuwa kuwa mbali na haki na kuikimbia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس