قُلِ ٱللَّهُ يُحۡيِيكُمۡ ثُمَّ يُمِيتُكُمۡ ثُمَّ يَجۡمَعُكُمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ لَا رَيۡبَ فِيهِ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَعۡلَمُونَ
Sema: Mwenyezi Mungu anakuhuisheni, kisha anakufisheni, kisha anakukusanyeni Siku ya Kiyama isiyo na shaka. Lakini watu wengi hawajui.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, uwaambie hawa washirikina wenye kukanusha kufufuliwa, “Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, Atawahuisha duniani kipindi Anachotaka muishi, kisha Atawafisha humo, kisha Atawakusanya mkiwa hai kwenye Siku ya Kiyama isiyokuwa na shaka.» Lakini wengi wa watu hawajui kwamba Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kuwafisha, kisha kuwafufua Siku ya Kiyama.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس