يَسۡمَعُ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ثُمَّ يُصِرُّ مُسۡتَكۡبِرٗا كَأَن لَّمۡ يَسۡمَعۡهَاۖ فَبَشِّرۡهُ بِعَذَابٍ أَلِيمٖ
Anaye sikia Aya za Mwenyezi Mungu akisomewa, kisha anashikilia yale yale aliyo katazwa, na anajivuna, kama kwamba hakuzisikia. Basi mbashirie adhabu chungu!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Anayezisikia aya za kitabu cha Mwenyezi Mungu akisomewa kisha akaendelea kwenye ukanushaji wake kwa kujiona ni mkubwa zaidi wa kutoweza kumfuata Mwenyezi Mungu na Mtume wake, kama kwamba yeye hakusikia alichosomewa miongoni mwa aya za Mwenyezi Mungu. Basi mbashirie, ewe Mtume, huyo mrongo sana mwenye dhambi nyingi adhabu yenye uchungu inayoumiza ndani ya Moto wa Jahanamu Siku ya Kiyama.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس