وَلَوۡ قَٰتَلَكُمُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوَلَّوُاْ ٱلۡأَدۡبَٰرَ ثُمَّ لَا يَجِدُونَ وَلِيّٗا وَلَا نَصِيرٗا
Na lau makafiri wangeli pigana nanyi basi bila ya shaka wangeli geuza migongo, kisha wasingeli pata mlinzi wala msaidizi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau makafiri wa Makkah wangalipigana vita na nyinyi, wangalishindwa na nyinyi na wangaliwapa migongo yao kama vile anavyofanya anayeshindwa vitani, kisha hawatapata, asiyekuwa Mwenyezi Mungu, rafiki wa kushikana na wao kuwapiga vita nyinyi wala msaidizi wa kuwasaidia wao wapigane na nyinyi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس