سَمَّـٰعُونَ لِلۡكَذِبِ أَكَّـٰلُونَ لِلسُّحۡتِۚ فَإِن جَآءُوكَ فَٱحۡكُم بَيۡنَهُمۡ أَوۡ أَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡۖ وَإِن تُعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ فَلَن يَضُرُّوكَ شَيۡـٔٗاۖ وَإِنۡ حَكَمۡتَ فَٱحۡكُم بَيۡنَهُم بِٱلۡقِسۡطِۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُقۡسِطِينَ
Hao ni wasikilizaji kwa ajili ya kusema uwongo, na ni walaji mno vya haramu! Basi wakikujia, wahukumu baina yao au jipuuze nao. Na ukijipuuza nao, basi wao hawatakudhuru kitu. Na ukiwahukumu, basi hukumu baina yao kwa uadilifu. Hakika Mwenyezi Mungu anawapenda waadilifu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mayahudi hawa wanakusanya kati ya usikilizaji urongo na ulaji haramu. Basi watakapokujia wakishtakiana kwako, basi hukumu kati yao au waache. Na usipohukumu kati yao, hawataweza kukudhuru kwa chochote. Na iwapo utahukumu, basi hukumu kati yao kwa uadilifu. Hakika Mwenyezi Mungu Anawapenda waadilifu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس