إِنَّ ٱلۡمُصَّدِّقِينَ وَٱلۡمُصَّدِّقَٰتِ وَأَقۡرَضُواْ ٱللَّهَ قَرۡضًا حَسَنٗا يُضَٰعَفُ لَهُمۡ وَلَهُمۡ أَجۡرٞ كَرِيمٞ
Kwa hakika wanaume wanao toa sadaka, na wanawake wanao toa sadaka, na wakamkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mwema, watazidishiwa mardufu na watapata malipo ya ukarimu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika ya wale wanaume na wanawake wanaotoa sadaka kutokana na mali yao na wakatumia katika njia ya Mwenyezi Mungu matumizi zikiwa radhi nyoyo zao, kwa kutafuata radhi za Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, wataongezewa malipo mema ya hayo, na juu ya hayo watapata malipo mengi, nayo ni Pepo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس