ٱلَّذِينَ يَبۡخَلُونَ وَيَأۡمُرُونَ ٱلنَّاسَ بِٱلۡبُخۡلِۗ وَمَن يَتَوَلَّ فَإِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلۡغَنِيُّ ٱلۡحَمِيدُ
Ambao wanafanya ubakhili, na wanaamrisha watu wafanye ubakhili. Na anaye geuka, basi Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha, Msifiwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hawa wenye kujiona ndio wale wanaoyafanyia ubahili mali yao, wasiyatoe katika njia ya Mwenyezi Mungu, na wakawaamuru watu wawe mabahili kwa kuwapambia huo ubahili. Na yoyote anayezunguka nyuma kwa kuacha kumtii Mwenyezi mungu hamdhuru yoyote isipokuwa nafsi yake, na hatamdhuru Mwenyezi Mungu chochote, kwani Mwenyezi Mungu Ndiye Mkwasi Asiyehitajia viumbe vyake, Mwenye kuhimidiwa Ambaye Ana kila sifa njema iliyokamilika na kila tendo zuri ambalo Anastahiki kushukuriwa kwalo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس