لَأَنتُمۡ أَشَدُّ رَهۡبَةٗ فِي صُدُورِهِم مِّنَ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَوۡمٞ لَّا يَفۡقَهُونَ
Hakika nyinyi ni kitisho zaidi katika vifua vyao kuliko Mwenyezi Mungu. Hayo ni kwa kuwa hao ni watu wasio fahamu kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kwa hakika, hofu ya wanafiki na Mayahudi kuwaogopa nyinyi, enyi Waumini, ni kubwa mno ndani ya nyoyo zao kuliko vile wanavyomuogopa na kumcha Mwenyezi Mungu. Hii ni kwa sababu ya kuwa wao ni watu wasiouelewa utukufu wa Mwenyezi Mungu na kuwa na Imani Kwake, na hawaogopi mateso Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس