لَّهُمۡ عَذَابٞ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَشَقُّۖ وَمَا لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ مِن وَاقٖ
Wanayo adhabu katika maisha ya dunia, na adhabu ya Akhera hapana shaka ina mashaka zaidi. Na wala hawatakuwa na wa kuwalinda na Mwenyezi Mungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Makafiri hawa wenye kuzuia njia ya Mwenyezi Mungu watakuwa na adhabu ngumu katika maisha ya ulimwenguni kwa kuuawa, kutekwa na kuhiziwa. Na kwa hakika, adhabu yao huko Akhera ni nzito zaidi na ni kali zaidi, na hawatakuwa na kizuizi chenye kuwazuia wasipate adhabu ya Mwenyezi mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس