لَّقَدۡ أَنزَلۡنَآ ءَايَٰتٖ مُّبَيِّنَٰتٖۚ وَٱللَّهُ يَهۡدِي مَن يَشَآءُ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Kwa yakini tumeteremsha Ishara zinazo bainisha. Na Mwenyezi Mungu hummwongoa amtakaye kwenye Njia Iliyo Nyooka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kwa hakika tumeteremsha katika Qur’ani vitambulisho vilivyo waziwazi venye kuongoza kwenye haki. Na Mwenyezi Mungu Anamuongoza na kumuelekeza Anayemtaka katika waja wake kwenye njia iliyolingana sawa, nayo ni Uislamu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس