وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا لُقۡمَٰنَ ٱلۡحِكۡمَةَ أَنِ ٱشۡكُرۡ لِلَّهِۚ وَمَن يَشۡكُرۡ فَإِنَّمَا يَشۡكُرُ لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَنِيٌّ حَمِيدٞ
Na tulimpa Luqman hikima, tukamwambia: Mshukuru Mwenyezi Mungu. Na mwenye kushukuru basi hakika anashukuru kwa manufaa ya nafsi yake. Na aliye kufuru, basi Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Msifiwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kwa hakika tulimpa mja mwema miongoni mwa waja wetu , naye ni Luqman, busara, nayo ni ufahamu wa Dini, akili na usawa wa maneno, na tulimwambia, «Zishukuru neema za Mwenyezi Mungu juu yako. Na Mwenye kumshukuru Mola wake, faida yake itamrudia mwenyewe, na Mwenye kukanusha neema Zake, basi Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Hahitaji kushukuriwa, ni Zake Yeye shukrani na sifa njema kwa kila hali.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس