ذَٰلِكُم بِمَا كُنتُمۡ تَفۡرَحُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّ وَبِمَا كُنتُمۡ تَمۡرَحُونَ
Haya ni kwa sababu mlikuwa mkijitapa katika ardhi pasipo haki, na kwa sababu mlikuwa mkijishaua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Adhabu hiyo itakayowapata ni kwa sababu ya kughafilika mliokuwa nako katika uhai wenu wa kilimwengu, kwa kuwa mlikuwa mkifurahika na yale mnayoyatenda ya maasia na madhambi na tabia mliokuwa nazo za gogi, kiburi na kuwafanyia udhalimu waja wa Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس