۞يَوۡمَ يَجۡمَعُ ٱللَّهُ ٱلرُّسُلَ فَيَقُولُ مَاذَآ أُجِبۡتُمۡۖ قَالُواْ لَا عِلۡمَ لَنَآۖ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّـٰمُ ٱلۡغُيُوبِ
Ile siku ambayo Mwenyezi Mungu atapo wakusanya Mitume awaambie: Mlijibiwa nini? Watasema: Hatuna ujuzi; hakika Wewe ndiye Mjuzi Mkubwa wa yote yaliyo fichikana.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ikumbukeni, enyi watu, Siku ya Kiyama, siku Mwenyezi Mungu atakapo kuwakusanya Mitume, amani iwashukie, na awaulize kuhusu majibu ya watu wao waliyoyapata, pindi walipowalingania kwenye tawhīd (kumpwekesha Mwenyezi Mungu). Na wao watajibu, «Hatuna ujuzi, sababu hatuyajui yaliyomo ndani ya nyoyo za watu wala yale waliyoyazua baada yetu. Hakika yako wewe ni Mjuzi wa kila kitu kilichofichika na kilicho wazi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس