قَالُواْ نُرِيدُ أَن نَّأۡكُلَ مِنۡهَا وَتَطۡمَئِنَّ قُلُوبُنَا وَنَعۡلَمَ أَن قَدۡ صَدَقۡتَنَا وَنَكُونَ عَلَيۡهَا مِنَ ٱلشَّـٰهِدِينَ
Wakasema: Tunataka kukila chakula hicho, na nyoyo zetu zitue, na tujue kwamba umetuambia kweli, na tuwe miongoni mwa wanao shuhudia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ḥawāriyyūn wakasema, «Tunataka kula kutoka kwenye meza hiyo, nyoyo zetu zipate kutulia kwa kuishuhudia, tupate kujua kwa yakini ukweli wako kuhusu unabii wako na tupate kuwa ni wenye kuishuhudia miujiza hii kwamba Mwenyezi Mungu Ameiteremsha iwe ni hoja kwetu juu ya upweke Wake na uwezo Wake kufanya Alitakalo na pia iwe ni hoja kwako juu ya ukweli kuhusu unabii wako.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس