وَقَفَّيۡنَا عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِم بِعِيسَى ٱبۡنِ مَرۡيَمَ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ مِنَ ٱلتَّوۡرَىٰةِۖ وَءَاتَيۡنَٰهُ ٱلۡإِنجِيلَ فِيهِ هُدٗى وَنُورٞ وَمُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ مِنَ ٱلتَّوۡرَىٰةِ وَهُدٗى وَمَوۡعِظَةٗ لِّلۡمُتَّقِينَ
Na tukawafuatishia hao Isa bin Maryamu kuyahakikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na tukampa Injili iliyomo ndani yake uwongofu, na nuru na inayo sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na uwongofu na mawaidha kwa wachamngu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na tukawafuatishia, Manabii wa Wana wa Isrāīl, ‘Īsā mwana wa Maryam akiwa ni mwenye kuyaamini yaliyomo ndani ya Taurati na kuzitumia hukumu zilizomo kati ya zile ambazo hazikufutwa na Kitabu chake na tukamteremshia Injili ikiwa ni yenye kuongoza kwenye haki na yenye kuyaeleza yale ambayo watu hawakuyajua katika hukumu za Mwenyezi Mungu na ni yenye kutoa ushahidi juu ya ukweli wa Taurati kwa hukumu zake ilizokusanya Na tumeifanya ni bainifu kwa wale wanaomuogopa Mola wao, ni yenye kuwakemea wasiyafanye yaliyoharamishwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس