تَرَىٰ كَثِيرٗا مِّنۡهُمۡ يَتَوَلَّوۡنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ لَبِئۡسَ مَا قَدَّمَتۡ لَهُمۡ أَنفُسُهُمۡ أَن سَخِطَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ وَفِي ٱلۡعَذَابِ هُمۡ خَٰلِدُونَ
Utawaona wengi wao wanafanya urafiki na walio kufuru. Hakika ni maovu yaliyo tangulizwa na nafsi zao hata Mwenyezi Mungu amewakasirikia, nao watadumu katika adhabu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Utawaona, ewe Mtume, wengi wa hawa Mayahudi wanawafanya washirikina kuwa ni wategemewa wao. Ni baya mno hilo walilolifanya la mshikamano huo uliokuwa ni sababu ya kukasirikiwa kwao na Mwenyezi Mungu na kukaa kwao milele kwenye adhabu ya Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس