وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ وَٱحۡذَرُواْۚ فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ
Na mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume, na tahadharini. Na ikiwa mtageuka basi jueni ya kuwa juu ya Mtume wetu ni kufikisha ujumbe tu ulio wazi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Fuateni amri, enyi Waislamu, ya kumtii Mwenyezi Mungu na kumtii Mtume Wake Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, katika kila mnalolifanya na mnaloliacha. Na mcheni Mwenyezi Mungu na mumtunze katika hayo. Na mkikataa kufuata amri na mkayafanya mliyokatazwa, basi jueni kuwa jukumu la mjumbe wetu Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ni ufikishaji ulio wazi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس