يُولِجُ ٱلَّيۡلَ فِي ٱلنَّهَارِ وَيُولِجُ ٱلنَّهَارَ فِي ٱلَّيۡلِۚ وَهُوَ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ
Anaingiza usiku katika mchana, na anaingiza mchana katika usiku. Na Yeye ni Mwenye kuyajua yaliomo vifuani.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Anazitia saa za usiku zilizopungua ndani ya mchana na hivyo basi mchana ukaongezeka, na Anazitia saa za mchana ndani ya usiku, na hivyo basi usiku ukaongezeka. Na Yeye , kutakasika ni Kwake, ni Mjuzi wa yaliyomo ndani ya vifua vya viumbe Vyake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس