وَٱسۡتَكۡبَرَ هُوَ وَجُنُودُهُۥ فِي ٱلۡأَرۡضِ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّ وَظَنُّوٓاْ أَنَّهُمۡ إِلَيۡنَا لَا يُرۡجَعُونَ
Na alipanda kiburi yeye na majeshi yake katika nchi bila ya haki, na wakadhania kuwa hawatarudishwa kwetu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Fir’awn na askari wake walifanya kiburi katika nchi ya Misri bila ya haki kwa kukataa kumuamini Mūsā na kumfuata katika lile alilowaitia na wakadhani kwamba baada ya kufa kwao hawatafufuliwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس