۞وَمَن يَقۡنُتۡ مِنكُنَّ لِلَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَتَعۡمَلۡ صَٰلِحٗا نُّؤۡتِهَآ أَجۡرَهَا مَرَّتَيۡنِ وَأَعۡتَدۡنَا لَهَا رِزۡقٗا كَرِيمٗا
NA MIONGONI mwenu atakeye mt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na akatenda mema, tutampa malipo yake mara mbili, na tutamwandalia riziki ya ukarimu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake kati yenu na akafanya matendo Aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu , tutampa malipo mema ya matendo yake mara mbili zaidi ya malipo ya asiyekuwa yeye kati ya wanawake wengine, na tumemuandalia yeye riziki nzuri, nayo ni Pepo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس