وَمِنَ ٱلنَّاسِ وَٱلدَّوَآبِّ وَٱلۡأَنۡعَٰمِ مُخۡتَلِفٌ أَلۡوَٰنُهُۥ كَذَٰلِكَۗ إِنَّمَا يَخۡشَى ٱللَّهَ مِنۡ عِبَادِهِ ٱلۡعُلَمَـٰٓؤُاْۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ غَفُورٌ
Na katika watu, na wanyama, na mifugo, pia rangi zao zinakhitalifiana. Kwa hakika wanao mcha Mwenyezi Mungu miongoni mwa waja wake ni wanazuoni. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na miongoni mwa watu na wanyama, ngamia, ng’ombe, mbuzi na kondoo tumeumba wakiwa rangi tofauti vilevile. Kati ya hao kuna wekundu, weupe weusi na wenye rangi nyinginezo, kama vile kutofautiana rangi za matunda na majabali. Hakika wanaomcha Mwenyezi Mungu na kujikinga na mateso Yake kwa kumtii na kujiepusha kumuasi ni wale wanaomjua Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake,sifa Zake na Sheria Zake, na uweza Wake juu ya kila kitu ambao miongoni mwavyo ni kutofautiana viumbe hivi pamoja na kuwa sababu yake ni moja, na wanayatia akilini yaliyomo ndani ya mawaidha na mazingatio. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mshindi Mwenye nguvu Asiyeshindwa, Mwingi wa kusamehe Anawapa malipo mema watiifu, na Anawasamehe.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس