وَهُمۡ يَصۡطَرِخُونَ فِيهَا رَبَّنَآ أَخۡرِجۡنَا نَعۡمَلۡ صَٰلِحًا غَيۡرَ ٱلَّذِي كُنَّا نَعۡمَلُۚ أَوَلَمۡ نُعَمِّرۡكُم مَّا يَتَذَكَّرُ فِيهِ مَن تَذَكَّرَ وَجَآءَكُمُ ٱلنَّذِيرُۖ فَذُوقُواْ فَمَا لِلظَّـٰلِمِينَ مِن نَّصِيرٍ
Na humo watapiga makelele: Mola wetu Mlezi! Tutoe tufanye mema sio yale tuliyo kuwa tukiyafanya. Kwani hatukukupeni umri wa kutosha kukumbuka mwenye kukumbuka? Na akakujieni Mwonyaji? Basi onjeni! Kwani walio dhulumu hawana wa kuwanusuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hawa makafiri watapiga kelele kwa ukali wa adhabu ndani ya Moto wa Jahanamu wakiomba kuokolewa, «Mola wetu! Tutoe kwenye Moto wa Jahanamu na uturudishe duniani tupate kufanya matendo mema ambayo siyo yale tuliokuwa tukiyafanya katika uhai wetu wa duniani, tupate kuamini badala ya kukanusha.» Hapo Mwenyezi Mungu Awaambie, «Kwani hatukuwapa katika kipindi cha uhai kadiri inayotosha ya umri kwa mwenye kutaka kuwaidhika awaidhike, na akawajia Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na pamoja na hivyo msiwaidhike? Basi onjeni adhabu ya Jahanamu! Kwani wenye kukanusha hawana msaidizi wa kuwaokoa na adhabu ya Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس