تَدۡعُونَنِي لِأَكۡفُرَ بِٱللَّهِ وَأُشۡرِكَ بِهِۦ مَا لَيۡسَ لِي بِهِۦ عِلۡمٞ وَأَنَا۠ أَدۡعُوكُمۡ إِلَى ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡغَفَّـٰرِ
Mnaniita nimkufuru Mwenyezi Mungu na nimshirikishe na yule ambaye simjui, nami nakuiteni kwa Mwenye nguvu Mwenye kusamehe?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Mnanilingania mimi nimkanushe Mwenyezi Mungu na nimshirikishe Yeye na kitu amabacho sina ujuzi nacho kuwa kinastahiki kuabudiwa badala Yake- na hili ni miongoni madhambi makubwa zaidi na maovu zaidi- Na mimi ninawalingania kwenye njia yenye kupelekea kwa Mwenyezi Mungu Aliye Mshindi katika kutesa Kwake, Mwingi wa msamaha kwa aliyerudia Kwake kwa kutubia baada ya kumuasi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس