۞وَٱذۡكُرۡ أَخَا عَادٍ إِذۡ أَنذَرَ قَوۡمَهُۥ بِٱلۡأَحۡقَافِ وَقَدۡ خَلَتِ ٱلنُّذُرُ مِنۢ بَيۡنِ يَدَيۡهِ وَمِنۡ خَلۡفِهِۦٓ أَلَّا تَعۡبُدُوٓاْ إِلَّا ٱللَّهَ إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Na mtaje ndugu wa kina A'di, alipo waonya watu wake kwenye vilima vya mchanga. Na kwa yakini waonyaji wengi walitokea kabla yake na baada yake kuwaambia: Msimuabudu isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Hakika mimi nakukhofieni isikupateni adhabu ya siku iliyo kuu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kumbuka, ewe Mtume, Nabii wa Mwenyezi Mungu Hūd, ndugu yao kina 'Ād kinasaba na siyo kidini, alipowaonya watu wake kuwa watashukiwa na adhabu ya Mwenyezi Mungu wakiwa kwenye nyumba zao hapo Aḥqāf (mahali kwenye mchanga mwingi) kusini mwa Arabuni. Na kwa hakika wamepita Mitume wakawaonya watu wao kabla ya Hūd na baada yake wakiwaambia, «Msimshirikishe Mwenyezi Mungu na kitu chochote mnapomuabudu. Mimi nawachelea nyinyi adhabu ya Mwenyezi Mungu katika Siku yenye kituko kikubwa , nayo ni Siku ya Kiyama.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس