Muhammad
ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَصَدُّواْ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ أَضَلَّ أَعۡمَٰلَهُمۡ
Walio kufuru na wakazuilia njia ya Mwenyezi Mungu, Yeye atavipotoa vitendo vyao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wale waliokataa kwamba Mwenyezi Mungu Ndiye Peke Yake Mungu wa kweli Asiye na mshirika, na wakawazuia watu na Dini Yake, Mwenyezi Mungu Atazifuta amali zao na kuzipomosha na Atawapa usumbufu kwa sababu ya amali zao hizo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس