فَلَا تَهِنُواْ وَتَدۡعُوٓاْ إِلَى ٱلسَّلۡمِ وَأَنتُمُ ٱلۡأَعۡلَوۡنَ وَٱللَّهُ مَعَكُمۡ وَلَن يَتِرَكُمۡ أَعۡمَٰلَكُمۡ
Basi msiregee na kutaka suluhu, maana nyinyi ndio mtakao shinda. Na Mwenyezi Mungu yu pamoja nanyi, wala hatakunyimeni malipo ya vitendo vyenu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Basi msiwe wanyonge, enyi wenye kumuamini Mwenyezi Mugu na Mtume Wake, wa kujiepusha na kupambana na washirikina, mkaogopa kupigana nao na mkawaita kwenye suluhu na masikilizano na hali ya kuwa nyinyi ndio wenye ushindi na nguvu juu yao, na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Yuko pamoja na nyinyi kwa kuwanusuru na kuwapa nguvu. Hapa kuna bishara kubwa ya kupatiwa ushindi na kusaidiwa juu ya maadui. Na Mwenyezi Mungu Hatawapunguzia nyinyi malipo mema ya matendo yenu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس