يَٰقَوۡمِ ٱدۡخُلُواْ ٱلۡأَرۡضَ ٱلۡمُقَدَّسَةَ ٱلَّتِي كَتَبَ ٱللَّهُ لَكُمۡ وَلَا تَرۡتَدُّواْ عَلَىٰٓ أَدۡبَارِكُمۡ فَتَنقَلِبُواْ خَٰسِرِينَ
Enyi watu wangu! Ingieni katika nchi takatifu ambayo Mwenyezi Mungu amekuandikieni. Wala msirudi nyuma, msije mkawa wenye kukhasirika.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Enyi watu wangu, Ingieni kwenye ardhi takatifu, yaani iliyotakaswa, nayo ni Bait al-Maqdis na sehemu zilizo kando-kando yake, ambayo Mwenyezi Mungu Ametoa ahadi muingie na mkapigane na makafiri waliyo humo wala msirudi nyuma mkaacha kupigana na hao majabari, kwani mkifanya hivyo mtaikosa heri ya duniani na heri ya Akhera.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس