وَمَن يَتَوَلَّ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ فَإِنَّ حِزۡبَ ٱللَّهِ هُمُ ٱلۡغَٰلِبُونَ
Na atakaye fanya urafiki na Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, basi hakika kundi la Mwenyezi Mungu ndilo lenye kushinda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu na akafuata muongozo wa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na akawa na muelekeo wa Waumini, basi yeye ni katika kundi la Mwenyezi Mungu, na kundi la Mwenyezi Mungu ndilo la washindi wenye kunusurika.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس