وَإِذَا نَادَيۡتُمۡ إِلَى ٱلصَّلَوٰةِ ٱتَّخَذُوهَا هُزُوٗا وَلَعِبٗاۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَوۡمٞ لَّا يَعۡقِلُونَ
Na mnapo adhinia Sala wao wanaichukulia maskhara na mchezo. Hayo ni kwa sababu wao ni watu wasio na akili.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na anapoadhini mwadhini wenu, enyi Waumini, kuita watu kwenye Swala, Mayahudi, Wanaswara na washirikina wanafanya shere na kuukejeli mwito wenu wa hiyo Swala. Hii ni kwa sababu ya ujinga wao wa kutomjua Mola wao na kwa kuwa wao hawajui uhakika wa ibada.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس