أَفَلَا يَتُوبُونَ إِلَى ٱللَّهِ وَيَسۡتَغۡفِرُونَهُۥۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Je! Hawatubu kwa Mwenyezi Mungu na wakamwomba msamaha? Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira na Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mbona Wanaswara hawa hawarudi kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na wakatubia kwa waliyoyasema na wakamuomba msamaha Mwenyezi Mungu Aliyetukuka? Kwani Mwenyezi Mungu , Aliyetukuka, ni Mwenye kuyasamehe madhambi ya wenye kutubia, ni Mwenye huruma kwao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس