وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَآ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَحِيمِ
Na wale walio kufuru na wakazikanusha Ishara zetu, hao ndio watu wa Motoni.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale ambao waliukanusha upweke wa Mwenyezi Mungu, wakaukataa unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na wakazikanusha aya Zake zilizoteremshwa kwa Mitume Wake, hao ndio watu wa Motoni wenye kukaa daima humo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس