يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تُحَرِّمُواْ طَيِّبَٰتِ مَآ أَحَلَّ ٱللَّهُ لَكُمۡ وَلَا تَعۡتَدُوٓاْۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡمُعۡتَدِينَ
Enyi mlio amini! Msiharimishe vizuri alivyo kuhalalishieni Mwenyezi Mungu, wala msikiuke mipaka. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wakiukao mipaka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi ambao mliamini, msiharamishe vizuri alivyowahalalishia Mwenyezi Mungu, miongoni mwa vyakula na vinywaji na kuoa wanawake, mkayatia mkazo mambo ambayo Mwenyezi Mungu Ameyatolea nafasi kwenu, na msipite mipaka ya vitu alivyoviharamisha Mwenyezi Mungu. Kwani Mwenyezi Mungu Hawapendi wenye kupita mipaka.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس