وَكُلُواْ مِمَّا رَزَقَكُمُ ٱللَّهُ حَلَٰلٗا طَيِّبٗاۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ ٱلَّذِيٓ أَنتُم بِهِۦ مُؤۡمِنُونَ
Na kuleni katika alivyo kuruzukuni Mwenyezi Mungu, halali na vizuri. Na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye mnamuamini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na mstarehe, enyi Waumini, kwa halali nzuri Aliyowapa Mwenyezi Mungu na kuwatunukia. Na mcheni Mwenyezi Mungu kwa kufuata amri Zake na kujiepusha na makatazo Yake. Kwani kumuamini kwenu Mwenyezi Mungu kunawalazimisha nyinyi kumcha Yeye na kumtunza[2].
____________________
[2]Neno la kiarabu hapa ni murāqabah lenye maana ya kuangalia kwa makini, kutunza, kuchunga, kulinda n.k. Makusudio hapa ni kuwa na yakini kuwa Mwenyezi Mungu Akuona, akusikia na azijua harakati zako zote, yakini ambayo inamfanya mtu amuogope Mwenyezi Mungu.Kwa maelezo zaidi, ang. 'Uthaimīn,M.S. Sharh Riy,ād al-Sālihīn, Vol. I, P.324
____________________
[2]Neno la kiarabu hapa ni murāqabah lenye maana ya kuangalia kwa makini, kutunza, kuchunga, kulinda n.k. Makusudio hapa ni kuwa na yakini kuwa Mwenyezi Mungu Akuona, akusikia na azijua harakati zako zote, yakini ambayo inamfanya mtu amuogope Mwenyezi Mungu.Kwa maelezo zaidi, ang. 'Uthaimīn,M.S. Sharh Riy,ād al-Sālihīn, Vol. I, P.324
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس