وَٱذۡكُرُوٓاْ إِذۡ أَنتُمۡ قَلِيلٞ مُّسۡتَضۡعَفُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ تَخَافُونَ أَن يَتَخَطَّفَكُمُ ٱلنَّاسُ فَـَٔاوَىٰكُمۡ وَأَيَّدَكُم بِنَصۡرِهِۦ وَرَزَقَكُم مِّنَ ٱلطَّيِّبَٰتِ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Na kumbukeni mlipo kuwa wachache, mkionekana wanyonge katika nchi, mnaogopa watu wasikunyakueni, naye akakupeni pahala pazuri pa kukaa, na akakutieni nguvu kwa nusura yake, na akakupeni riziki nzuri ili mpate kushukuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kumbukeni, enyi Waumini, neema za Mwenyezi Mungu juu yenu mlipokuwa ndani ya Maka ni wachache wa idadi mnanyanyaswa, mnaogopa msije mkanyakuliwa na makafiri kwa haraka, Akawapatia makao ya nyinyi kuhamia nayo ni Madina na akawapa nguvu kwa kuwapa ushindi juu yao siku ya Badr na Akawapa vyakula kati ya vitu vizuri ambavyo ngawira ni miongoni mwavyo, ili mumshukuru Yeye kwa alichowaruzuku nacho na kuwaneemesha.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس